Thursday, September 4, 2014

Umri wa ndoa uwe miaka 18- 21 -wanaharakati


Watu wanaoishi na changamoto za ulemavu wakifuatilia mjadala huo Dodoma


Baadhi ya Wajumbe wa Bunge maalum la Katiba wakifuatilia

Wajumbe wa Bunge maalum la Katiba wakisikiliza madai ya wananchi kwenye rasimu ya Katiba itakayojadiliwa Bungeni wiki hii

Uongozi wa Bungwe Maalum la Katiba mbadala (Bunge Kivuli) wakiendelea kuongoza Bunge hilo Mjini Ddodoma, Katikati ni Mwenyekiti wa Bunge hilo, Dk. Visencia Shule

Mmoja wa wasichana mwenye miaka 14 akipiga magoti kuonesha huruma kwa wanaanchi na wajumbe wa Bunge maalum la katiba kuwa wasikubali kuendelea kuruhusu wasichana wadogo kuolewa. wasichana hao walitoa tamko lao kulaani kitendo cha sheria ya ndoa ya mwaka 1971 kuendelea kutumika hadi leo inayoruhusu wasichana wenye umri wa miaka 14 kuolewa

kundi la wasichana kutoka mikoa mbalimbali wakiomba katiba mpya ikataze ndoa za utotoni

WANAHARAKATI wanaoshiriki kongamano la Katiba  la kujadili masuala ya kijinsia yanayotakiwa kuzingatiwa kwenye mjadala wa Bunge maalum la Katiba wamewataka wajumbe wa Bunge maalum la Katiba kuhakikisha katiba mpya itakayotengenezwa inatamka  umri wa  kuolewa au kuoa uwe miaka 18 hadi 21 ili kuwapa nafasi watoto wa kike kupata nafasi ya kusoma na kukua.
Wakizungumza wakati wakiendesha Bunge kivuli au Bunge maalum maalum la Katiba lililoandaliwa na TGNP Mtandao kwa kushirkiana na Mtandao wa Wanawake na katiba  mjini Dodoma,  wanaharakati hao wamesema kuwa  wajumbe wa Bunge maalum bila kujali tofauti zao za kijinsi wanapaswa kuhakikisha wanapigania haki ya mtoto wa kike kuwa salama na kutokuolewa kabla ya kukomaa akiwa na umri wa chini ya miaka 18.
Akizungumza Mwenyekiti wa Bunge maalum Mbadala la Katiba Dk. Vicensia Shule amesema kuwa  wananchi wote wanatakiwa kuunganisha nguvu wakati huu wa mchakato wa Bunge la Katiba kuhakikisha masuala muhimu ya wanawake nay ale ambayo yanatoa ulinzi kwa makundi yaliyoko pembezoni yanazingatiwa na kuingizwa kwenye katiba mpya.
“hakuna taifa ambalo ni tajiri au watu wake wameendelea bila kupata elimu,   na kuzingatia usawa wa kijinsia. Haya yote yatafanyika kama kuna elimu ya kutosha kwa wasichana na kama wataolewa  wakiwa watoto hawataweza kupata elimu”alisema Dk Shule.
Mshiriki kutoka shirika la Active Youth of Tanzania Mwanza, Amina Kisero alisema kuwa  sheria ya ndoa ya mwaka 1971, imeelza kuwa umri wa kuolewa kwa msichana ni miaka  14 au 15 wakati kanuni ya adhabu  siura ya sita  sheria za Tanzania namba 1 na 2(i)  kinaahalalisha kitendo cha ubakaji kwa kigezo cha kuolewa.
“Vipengele vyote hivi ni kikwazo kwa mustakabali wa ulinzi  wa haki za mtoto , na haki ya afya ya uzazi kwa mujibu wa sheria  ya mtoto ya mwaka 2009, tunataka kama katiba mpya itatambua na kuweka bayana juu ya ulinzi wa mtoto wa kike sheria hizi zitafungwa” a;lisema Kisero
Kwa upande wake Khadija Haddy ambaye pia ni mtaalam wa afya ya Jamii kutoka YAP alisema kuwa  mtoto wa kike mwenye umri wa chini ya miaka 18  maumbile yake hayana uwezo wa kupokea mabadiliko ya kubeba ujauzito na kuzaa  kwa wakati unaotakiwa.
Alisema kuwa ndo za utotoni zinasababisha tatizo kubwa la kuongezeka kwa magonjwa ya wanawake kutokana na maumbile yao kushindwa kubeba mabadiliko ya kimwili.
Kwa mujibu wa takwimu ya UNFPA  za mwaka 2013 tatizo la ndo za utotoni linakuwa kwa kasi nchini licha ya kampeni kubwa ya wananchi inayopigwa kupambana na hali hiyo. Wilaya ya Shinyanga ikiongoza kwa asilimia 59, Tabora asilimia 58,Mara asilimia 55, Dodoma asilimia 51 na lindi asilimia 45.
Kongamano hili linaandaliwa na Mtandao wa Wanawake na Katiba kwa kushirikiana na TGNP Mtandao mjini Dodoma na kuwashirikisha wanawake na wanaume na makundi yote  ya kijamii zaidi ya 200 na wajumbe wa Bunge maalum la Katiba.
Mwisho

No comments: