Sunday, August 31, 2014

Uwakilishi 50/50 Bungeni: Wasiwasi watanda kwa wanawake




Na Mwandishi Wetu
Kuna hofu kubwa miongoni mwa wanawake kuwa hoja ya usawa wa kijinsia wa 50/50 katika nafasi za maamuzi iliyoaninishwa kwenye rasimu ya pili ya Katiba mpya  inaweza kuondolewa kutokana na wajumbe wa  wabunge  la Katiba kutokuielewa.
Akizungumza kwenye Kongamano la  wanawake kutoka mikoa yote nchini Tanzania lililoandaliwa na Mtandao wa Wanawake na Katiba kwa kushirikiana na TGNP Mtandao mjini Dodoma Mwenyekiti wa Mfuko wa Wanawake Profesa Ruth Meena amesema kuwa  baada ya kukutana na wajumbe was Bunge maalum la Katiba na kujadiliana juu ya kuendelea kuzingatia masuala ya kijinsia katika mijadala inayoendelea kuanzia kesho Jumanne amesema wamebaini kuwa kuna masuala muhimu ya usawa wa kijinsia ambayo yameachwa.
“Tumefuatilia na kuwasikiliza, tumegundua kuwa wenyewe (wajumbe) hawaelewi maana halisi ya usawa wa kijinsia na dhana ya 50 kwa 50 ambayo imeainishwa kwenye rasimu. Hii inapaswa kuwa agenda muhimu sana ya kufuatilia katika kipindi hiki”alisema Prof. Ruth
Meena amesema kuwa mchakato umeanza kwa kukusanya maoni yao na kuwa na mambo ambayo yatawaunganisha wote. Mchakato huo uliibua mambo mengi haswa katika mabaraza ya Katiba. Mwanzo kabisa masuala ya wanawake yalikuwa 12, tunapaswa kuendelea kudai yasitupwe yote”alisema Profesa Ruth.

 Profesa Meena amesema kuwa kila siku wanawake 24 wanafariki wakijifungua, hivyo Mtandao wa wanawake na katiba wamesema kwamba kujifungua kusiwe ni hukumu la kifo.

Pia amesema kuwa ni lazima 50 kwa 50 katika uongozi izingatiwe.
Mjumbe wa Bunge maalum la katiba kwa tiketi ya taasisi ya elimu Dk.  Avemaria Semakafu, amesema kuwa yeye na wenzake walioko bungeni watahakikisha wanapigania agenda ya mwanamke kuwa na haki sawa kama mwananchi yoyote na kamwe hawatayumbishwa na agenda za wanasiasa.
Mshiriki Anna Kiombo kutoka Mbeya alisema kuwa  ni lazima haki za wanawa na kuheshimiwa katika katiba mpya.
“Ni lazima jamii ielewe kuwa hakuna maendeleo ya taifa lolote bila kuwa na katiba inayozingatia uasawa wa kijinsia na haki za wanawake kutambulika, wanawake wa vijijini tunateseka na kunyanyasika kwabsabu hatutambuliki kwenye katiba mpya”alisema.
Leo jumanne umati huo wa wanawake utaendesha Bunge mbadala mjini hapa kwa lengo la kuyapa makundi yote ya wanawake nafasi  ya kueleza madai yao kwenye Bunge halisi linaloendelea mjini Dodoma.
Akizungumza aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao Usu Mallya amesema kuwa wameamua kuendesha Bunge mbadala mjini Dodoma ili kuamsha  uelewa na umakini kwa wananchi zaidi kuendelea kufuatilia mchakato,  kutoa fursa kwa wananchi wengine  kupaaza sauti zao  nje ya Bunge maalum,  kuonesha jinsi ambavyo wangependa Bunge hilo liendeshwe.
Aidha Bunge mbadala litasaidia kuonesha masuala ya kijinsia ambayo hayajazingatiwa kikamilifu na kudai yaingizwe kwenye katiba kwa muda huu uliobaki.
Mashirika mengine ambayo yanashiriki ni TAMWA, Oxfam, WILDAF,KIVULINI na mengine kutoka mikoa mbalimbali.

No comments: