Friday, September 12, 2014

MAJADILIANO YA MAPENDEKEZO YA KAMATI BUNGE MAALUM LA KATIBA KIKAO CHA 36-37



MTANDAO WA JINSIA TANZANIA - (TGNP)  
  MAJADILIANO YA MAPENDEKEZO YA KAMATI BUNGE MAALUM LA KATIBA      
 KIKAO CHA 36-37
Katika bunge la 36 na 37 lilianza rasmi kujadili rasimu ya katiba na Mwenyekiti wa bunge maalum la katiba mheshimiwa Samwel Sitta aliwaelekeza Wajumbe kujikita katika  majadiliano kwa kuzingatia sura ya 9 na 15 ambazo zinahusu Kuundwa na madaraka ya bunge la jamhuri ya muungano na Ulinzi na usalama wa Jamhuri ya Muungano, sambamba na kujadili sura mpya ambayo haikuwepo katika rasimu nayo ni  sura ya uchumi na maendeleo, utawala,Muundo wa serikali na muungano. Haya ndiyo maeneo walioelekezwa wajumbe kujikita katika majadiliano yao na kujenga hoja ambazo zinagusa maeneo hayo .
 Mwelekeo wa majadiliano ulijikita zaidi kwenye masuala yafuatayo: Wajumbe wengi walipendekeza kuwepo na kipengele ambacho kitatambulika kikatiba ambacho kitaruhusu haki ya kugoma kama wafanyakazi au watu wengine wowote ambao watakua na sababu za msingi za kufanya hivyo, mgomo wao utambulike kuwa halali na bunge litatunga sheria itayoongoza uwepo na usimamizi wa kipengele hicho.Na hii inaweza kuwekwa chini ya ibara ya 36 ambayo inazungumza juu ya haki ya mfanyakazi.

Hata hivyo, wajumbe walionekana kuelekeza majadiliano yao kwenye Ibara ya 47ambayo inazungumzia  haki ya mwanamke wakiongozwa na Mheshimiwa, Avemarie Semakafu na Doreen Maro, wajumbe walipendekeza kiongezwe  kipengele (h) ambacho kipekee kitazungumzia haki ya  kupata huduma bora na salama ya uzazi bure ili kuepusha vifo vingi vinavyotokana na ujauzito. Pia wajumbe walipendekeza kiongezwe kipengele (i) ambacho kitazungumzia haki ya mwanamke mjamzito kulindwa na kazi ngumu zinazohatarisha maisha yake na ya mtoto aliye tumboni. Na ili kulisimamia hili bunge litatunga sheria ambayo itasimamia na kuelekeza utekelezaji wa haki hii.
 Hoja nyingine iliyozungumzwa sana ni kuhusu suala la mahakama ya kadhi kwa Waislamu, suala hili lilijadiliwa sana  na wajumbe waliowengi na wajumbe walitofautiana, lakini wengi walipendekeza kwamba suala la mahakama ya kadhi libaki chini ya ibara ya 32 ambayo inahusu uhuru wa imani ya dini kwani taifa letu halina dini na kama tutaanza kuingiza masuala ya dini kwa upande mmoja katika  katiba tutakua hatujawatendea haki upande mwingine ambao ni wa wakristo.
Vilevile suala la  Haki ya mtoto lilijadiliwa sana na wajumbe walio wakiongozwa na Mheshiwa:Mary Mwanjelwa, Avemarie Semakafu, Askofu Thomas Maige, Paul Mapunda, wengi walipendekeza kuwepo na kipengele ambacho kitafafanua mtoto ni kuanzia miaka mingapi, ili kuondoa tatizo la unyanyasaji kwa watoto suala ambalo limekua sugu katika taifa letu na limeathiri watoto wengi.
Suala la 50/50 nalo lilizungumzwa sana na wabunge walio wengi wakiongozwa na Mheshimiwa: Doreen Maro,Faustina, na kukubaliana litambulike na liingizwe katika katiba na bunge litatunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa suala hili. Suala hili linaweza kuongezewa kipengele chini ya ibara ya 47 ambayo inazungumzia masuala ya haki za wanawake.
Kwa kiasi kikubwa majadiliano yaligusa masuala mbalimbali ya kijinsia na wajumbe waliowengi walionekana kuwa na uelewa kuhusu masuala ya jinsia maana kila mara mjumbe aliposimamam kuelezea hoja Fulani alikua akitamka maneno uwiano wa kijinsia,jinsia na uzingatiaji wa makundi yote.Hivyo basi hii inatoa taswira ya jitihada ya mapendekezo yaliyotolewa na asasi mbalimbali zinazotetea haki za wanawake ikiwepo Jukwaa la Wanawake na Katiba.       



No comments: