Wednesday, August 6, 2014

Wasanii watakiwa kutumia ngazi zao kukomesha mfumo dume


kaimu Mkurugenzi Mtendaji TGNP, Bi. Lilian Liundi akizungumza na wasanii kutoka sehemu mbalimbali jijini Dar es salaam


Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji TGNP, Usu mallya alitoa darasa kwa wasanii namna ya kuandaa kazi kwa kuzingatia uasawa wa Kijinsia na kupigania haki ya kuwa na bajeti yenye mrengo wa kijinsia ili kukidhi mahitaji ya kijinsia kwa makundi yote

usu Akiendelea

Wasanii wakifuatilia mafunzo hayo kwa umakini mkubwa

Wasanii waliofika wakiwa wametulia

Wasanii walioshiriki wakiwa kwenye makundi kujadili zaidi baada ya mtoa mada kuwapa fursa ya kubunga bongo

wasanii walipata fursa ya kutoa maoni yao kwa wanahabari waliofika kwaajili ya coverage ya tukio hilo

WASANII wametakia kutumia nafasi wanazopata kupanda majukwaani kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia na kudai uwajibikaji  na upatikanaji wa huduma za kijamii .
Akizungumza na wasanii  walioshiriki warsha ya siku moja ya TGNP iliyolenga kuwajengea uwezo wasanii kutumia nafasi yao katika kudai uwajibikaji, uandaaji wa bajeti kwa mrengo wa kijinsia na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia jijini Dar es salaam Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa TGNP Mtandao, Lilian Liundi amesema kuwa  wanasanii wana nafasi kubwa ya kutoa elimu, kuburudisha, kuonya na kukemea na kuleta  mabadiliko chanya.
Amewataka kutumia ipasavyo fursa walio nayo kuhakikisha wanapata  uelewa wa masuala yanayowagusa wananchi na kuandaa kazi zitakazosaidia kuleta mabadiliko, kama filamu, Michezo ya majukwaani, mashairi, ngoma, na uchoraji wa vibonzo.
“TGNP Mtandao tunafanya kazi na vyombo vya habari kwa muda mrefu, wasanii tunawatambua kama watoa taarifa pia, na mtindo wao wa utoaji wa taarifa ni wa haraka na unapendwa na wengi, ndio manaa tunakutana na wasanii kwaajili ya kuwawezesha kutumia fursa walizo nazo kupaaza sauti juu ya changamoto za kijamii”alisema Liundi
Alisema kuwa kila msanii ana hadhira yake  na kama atakuwa na uelewa juu ya masuala ya bajeti kwa mrengo wa kijinsia, akijua masuala muhimu yanauyohusu mgawanyo sawa wa rasilimali hasa kwa makundi yaliyoko pembezoni, akajengewa uwezo wa kufanya uchambuzi wa majukumu ya kijinsia na mahitaji muhimu  lazima jamii itabadilika na watendaji au watunga sera nao watapata ujumbe na kuleta mabadiliko.
Kwa upande wake Mwanachama  na aliyekuwa Mkurugenzi  Mtendaji wa TGNP Mtandao Usu Mallya, alisema kuwa  Utandawazi  na soko huria ambavyo vimeingia kuanzia miaka ya 1990 vimeipelekea serikali kupunguza wajibu wake wa kusimamia uchumi, ajira, masoko na biashara, sekta binafsi imepewa majukumu makubwa zaidi ya kuwa injini ya kutafuta biashara na masoko na kupelekea kuongezeka kwa tabaka  na wanawake wamezsidi kubaki nyuma kiuchumi.
“ Tunahitaji sana nguvu ya wasanii katika kuelimisha jamii na kushinikiza mabadiliko. Mwanamke kujitoa kwenye umasikini ni kazi ngumu sana, pamoja na majukumu aliyo nayo lakini bado hana maamuzi kuhusu fedha za kutekeleza majukumu aliyo nayo”alisema Usu
Kwa upande wake Stara Thomas, mwimbaji wa siku nyingi alisema kuwa  katika semina hiyo amepata mamabo makubwa ikiwa ni pamoja na kuuelewa mfumo dume ni kitu gani na jinsi unavyoadhiri maendeleo ya jamii hasa wanawake na watoto.
“katika semina hii nimejifunza kitu kikubwa, nimeelewa maana ya mfumo dume na jinsi unavyoadhiri jamii,  nitatumia elimu hii katika kazi zangu za sanaa ili kuleta mabadiliko”alisema Thomas
Naye Mwimbaji Irene Sanga, alisema kuwa wasanii wanatakiwa kuitumia nafasi waliyo nayo kuandaa kazi ambazo  zitafikisha ujumbe  wa kuleta mabadiliko sio mapenzi pekee. “sisi tuna nguvu tunaweza kuleta mabadiliko,  bila wasanii hakuna sherehe wala misiba, tunauwezo mkubwa wa kujibadilisha na kubeba uhusika wa kila aina tutumie vizuri fursa hizi.
Mwisho


No comments: