Thursday, December 8, 2011

Sheria Kandamizi Zirekebishwe -Waziri

WAZIRI wa Katiba na Sheria, Celina Kombani amesema iko haja ya kufanya utetezi na ushawishi kwa kurekebisha sheria na sera zote ambazo haziendani na mikataba mbalimbali ya kimataifa ya haki za binadamu zikiwemo za wanawake.

Alisema hayo katika uzinduzi wa machapisho mbalimbali ya Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) uliofanyika katika ofisi za kituo hicho zilizopo Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Alisema wakati huu ambapo bado kuna migongano mingi ya sheria, wameona vyema ukafanyika ushawishi na marekebisho ya pamoja katika mkataba wa kuondoa aina zote za ubaguzi dhidi ya wanawake, kama ilivyokubaliwa katika maazimio ya ulingo wa Beijing, Malengo ya Maendeleo ya Millenia na mikataba mingine ya kimataifa ambayo nchi imeridhia.

Alisema mwanamke amekuwa ni mtu wa kunyanyasika katika suala zima la mirathi kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo mila na desturi potofu zinazoendelea kutumika nchini.

Awali Mkurugenzi wa Bodi ya Wakurugenzi ya WLAC, Nakaziel Tenga alisema machapisho yaliyozinduliwa ni sehemu ya harakati za kumkomboa mwanamke katika mfumo dume uliogubika jamii ambapo mwanamke amekuwa hapati thamani iliyo sawa na mwanamume.

No comments: