Monday, June 2, 2014

TGNP Mtandao yawanoa washiriki wa MAISHA PLUS kijijini


Wawezeshaji kutoka TGNP weakijadiliana na wasimamizi wa MAISHA PLUS  hapo kijijini kabla ya kuanza kufundisha


wanakijiji wa MAISHA PLUS wakiwa tayari wamekaa wakisubiri kupata darasa kutoka TGNP

Wawezeshaji kutoka TGNP Deo Temba na Agnes Lukanga wakikaribishwa na 'Babu' wa  MAISHA PLUS  kijijini

"babu" akisisitiza jambo kuhusu darasa la TGNP kijijini

 Babu ni lazima achekeshe na kuingiza utani kwenye utambulisho

Deo temba kutoka TGNP akiwezesha kijijini hapo

Mshiriki wa MAISHA PLUS  kutoka Uganda akichangia  hasa kueleza uingizaji wa masuala ya kijinsia kwenye mchanakto wa kuandaa bajeti za kitaifa

Mwezeshaji Agness Lukanga akiwezesha

Mshiriki wa MAISHA PLUS kutoka Burundi akichangia

Mshiriki wa MAMA SHUJAA  kijijini akichangia


Wanawake wanashiriki kama walezi wa vijana na wakijifunza zaidi masuala ya kilimo na wanawake

washiriki wakiwa na wawezeshaji wakiwa na  bango la TGNP linaloonesha mzigo anaoubeba mwanamke  kutokana na kutokuwa na bajeti yenye jicho la kijinsia na mchango wake kutokutambuliwa. bango hilo liliibua mdajala mpana  na washiriki wote kutoka nchi za Afrika ya mashariki walisema tatizo lipo nchi zote

Na TGNP Staff
Mtandao wa Jinsia  Tanzania (TGNP),  imepata fursa ya kuwawezesha na kuwanjengea uwezo washiriki wa programu ya Maisha Plus na mama shujaa inayofanyika kila mwaka mara moja.
Katika uwezeshaji huo ambao uliwezeshwa na  wafanyakazi wa TGNP Mtandao  uliwawezesha washiriki hao kuibua mijadala kuhusu  ushiriki wa jamii katika kuandaa bajeti ya mrengo wa Kijinsia na ushiriki wa wananchi wa pembezobi katika kaundaa bajeti na ibebe masuala ya wananchi hasa wanawake.
Pilika pilika zilionekana katika kijiji cha Maisha Plus ambapo wanakijiji walionekana wakishughulisha na shughuli binafsi za kifamilia, kubadilishana mawazo na uzoefu walionao. Pia waliweza kupata darasa kutoka kwa wawezeshaji kutoka TGNP  Mtandao.
 Lengo la darasa hili ni kuwawezesha washiriki wa Maisha Plus vijana na mama shujaa wa chakula kutambua na kuelewa masuala ya kijinsia kwenye shughuli zao za kazi wanazozifanya kwani washiriki wanatoka sehemu mbalimbali na wanajishughulisha na kazi tafauti ambazo zinatofautiana wengine ni wasanii, waandishi wa habari, wafanyakazi wa taasisi mbalimbali, wengine bado ni wanafunzi wanaendelea na masoma.
Tunajua kwamba wakipata masuala muhimu ya kutetea usawa wa kijinsia na wanayaelewa huko wanapofanya kazi zao baadaye watayatumia vizuri sana na wataweza kuleta mabadiliko katika nchi yetu ndiyo maana tumeshiriki kwa pamoja kuhakikisha kwamba tunawajengea uwezo kwenye kampeni ya ‘Haki ya Kiuchumi: Rasilimali Ziwanufaishe Wanawake Walioko Pembezoni’ alisema Deogratius Temba, Afisa Habari wa TGNP Mtandao.
Aliendelea na kusema kuwa tumefurahi sana kuwepo na mjadala huu mpana kupitia picha chokozi na kuona ni fursa pekee kuendelea kusambaza kampeni ya Haki ya Uchumi kwa jamii nzima mjini na huko vijijini kwasababu watu walio vijijini ni wengi  na watakapoenda kule wataendeleza hii kampeni na lubadilisha jamii yetu ya kitanzania.
Suala la na mfumo dume na umiliki wa ardhi limejitokeza wakatii wa majadiliano kwani mfumo dume na umiliki wa uchumi vinashirikiana kwamba kama kuna mfumo dume mwanamke na kijana hawawezi kumiliki uchumi hivyo kuendelea  kubeba mzigo mkuwa wa kulea familia.
Wanakijiji wa Maisha Plus walifurahishwa na mjadala huu kwani una nia ya kumkomboa mwanamke kutokana na yale majukumu mazito anayokuwanayo nyumbani na jamii nzima inayomzunguka na kuwa na haki ya kumiliki ardhi na siyo kuwa mzalishaji pekee kama ilivyo sasa katika jamii nyingi hapa nchini. Vile vile wameweza kuona umuhimu wa kuhudhuria vikao vya kijiji ambapo wanaweza kupata fursa ya kutoa maoni na kushiriki moja kwa moja katika mchakato wa bajeti ya serikali kupitia serikali ya mtaa ambapo wengi wao hawakuwa na ufahamu huo.
Mama shujaa pia walitoa uzoefu wao kuhusu nafasi ya mwanamke katika jamii wanazotoka na kusema kuwa umiliki wa ardhi kwa kinamama bado ni changamoto kwani wengi wao wamebaki kuwa wazalishaji tu na kutumia ile ardhi na siyo kumiliki jambo ambalo linarudisha nyuma juhudi za kinamama katika kujikomboa kiuchumi. Vile vile walipongeza waandaaji kwa kuwa na mpango wa kutoa mafunzo mbalimbali yatakayowasaidia washiriki katika sehemu walizotoka na jamii kwa ujumla.

No comments: