Chimbuka la Kampeni hii ya kuzuia ukatili dhidi ya wanawake ni makubaliano yaliyopo katika kifungu cha utekelezaji cha 113 cha Mkutano Mkuu wa wanawake uliofanyka Beijing China mwaka 1999. Mkutano huu uliazimia kukomesha unyanyasaji dhidi ya wanawake kutokana na ripoti kuonyesha unyanyasaji dhidi ya wanawake ni moja kati ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu duniani. Tafiti inaonyesha, mmoja kati ya wanawake watatu hunyanyaswa kwa namna moja ama nyingine katika kipindi cha maisha yao.
Rejea; http://www.unifem.org/gender_issues/violence_against_women/
Mwaka huu baraza la umoja wa mataifa, liliridhia mapendekezo ya kukomesha unyanyasaji wa wanawake na kuanzishwa kwa kampeni ya kuzuia ukatili dhidi ya wanawake duniani kote. Nchini Tanzania Kampeni hii ilizinduliwa rasmi kitaifa na Mh. rais J. M Kikwete May 24, 2008.
Wachangiaji waliweza kubainisha Changamoto mbalimbali katika kufika malengo ya kampeni hii ambazo ni pamoja na;
Changamoto ya mila na desturi za baadhi ya makabila hapa nchini zinazoendeleza unyanyasaji wa wanawake kwa makusudi ama bila kukusudia- kwa mfano mila za ukeketaji, kurithisha wanawake, kupiga wanawake n.k. Pili ni Upatikanaji wa taarifa za ukatili dhidi ya wanawake- wengi wa wahanga hawaripoti vitendo vya ukatili wanavyotendewa na waume zao ama watu wengine, pia mara nyingi kesi zilizoripotiwa polisi hufutwa ama kumalizwa nje ya vyombo vya sheria kwa wahanga kuwasamehe watuhumiwa. Tatu, uelewa mdogo wa jamii juu ya kupambana na ukatili dhidi ya wanawake, kitu ambacho kinashawishi kuwepo na mpango maalumu wa kuielimisha zaidi jamii yetu. Hali ya kiuchumi pia imeelezwa kuwa ni changamoto mojawapo inayowasababisha wanawake wengi kunyanyasika na kushindwa kujitetea dhidi ya manyanyaso hayo. Hivyo kampeni hii itafanikiwa vizuri zaidi endapo kutakuwepo na mkakati wa kuwawezesha wanawake kiuchumi ili kuweza kujitegemea katika maamuzi mbalimbali juu ya maisha yao.
Mapendekezo yaliyofikiwa na Wanasemina ni;
1. Kutangaza kampeni hii katika vyombo vya habari- Tv, redio, magazeti na blogu, na tovuti mbalimbali ili wananchi wengi zaidi waweze kujiunga nayo na hivyo kufanikisha malengo yake.
2. Kuwe na mpango maalumu wa kuwawezesha wanawake kujitegemea kiuchumi.
3. Polisi walielimishwe na kuacha kumaliza kesi za unyanyasaji wa wanawake vituoni na kuendelea kulea tabia hii. Pia kuwepo na mtu maalumu anayehusika na maswala yote ya jinsia “Gender Focal Person” katika vituo vya polisi atakayehusika na kesi na maswala yote yanayohusiana na unyanyasaji wa wanawake.
4. Majaji wapatiwe mafunzo ya jinsia ya awali yaweze kuwasaidia katika kazi zao.
No comments:
Post a Comment