Wednesday, October 2, 2013

TATHMINI YA TAMASHA LA JINSIA 2013

SEMINA ZA JINSIA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (GDSS) 25/09/2013 ILIYOFANYIKA VIWANJA VYA TGNP MTANDAO

MADA:                      Tathmini ya Tamasha la Jinsia 2013
MWEZESHAJI:         Mary Nsemwa kutoka TGNP
WASHIRIKI:             66       (39 Ke/27 Me)

Mchakato:
Mwezeshaji aliwapitisha washiriki kwenye malengo makuu ya Tamasha la Jinsia 2013, na kisha kuwapitisha kwenye kazi za Kamati mbali mbali zilizokuwa zimeundwa zifanye kazi kabla na wakati wa Tamasha, ili kuhakikisha malengo ya Tamasha yanafikiwa.
Kisha, washiriki waligawanyika kwenye vikundi vinne kujadili Kamati nne tofauti kwa kuangalia mambo yafuatayo:
·        Mafanikio makubwa matatu kwa Kamati husika
·        Maeneo ya kuboresha na njia mahsusi tatu za kuboresha
·        Ushiriki wa wana GDSS kwenye Tamasha lijalo uboreshwe vipi.
Kamati za Tamasha la Jinsia 2013 zilizofanyiwa uchambuzi ni:
·        Kamati Kuu
·        Kamati ya Utafutaji Rasilimali na Utawala
·        Kamati ya Ushiriki
·        Kamati ya Habari, Taarifa na Mawasiliano
Kwa ujumla wa Kamati zote nne zilizojadiliwa, mambo yafuatayo yalijitokeza kutoka kwenye vikundi hivi vinne kama mafanikio:
·        Kwa kuingiza Bunge la Wananchi na Mahakama ya Wazi; maudhui ya Tamasha la mwaka huu yalikuwa  tofauti  yenye ubunifu  uliohamasisha ushiriki wa hali ya juu  tofauti na  miaka mingine;
·        Watoa mada za msingi (plenary) walikuwa mahiri, na warsha zilitumia mbinu shirikishi (uraghbishi) zilizofanya ushiriki kuwa mkubwa na mpana.
·        Washiriki wote kupatiwa chakula ilisaidia kutulia  na  bila kupoteza muda kwenda kutafuta chakula.
·        Washiriki wote kushiriki kikamilifu na kuchangia mijadala
·        Vikundi vya sanaa  vilifanya sanaa zenye maudhui  yanayoendana na mada  na  kuibua  mjadala mkubwa.
·        Tamasha lilifanikiwa kutangazwa sana kwenye redio, televisheni, mitandao ya kijamii, magazetini n.k. kabla, wakati na baada ya Tamasha
Maeneo yafuatayo yalitajwa kuhitaji maboresho kwenye matamasha yajayo:
·        Idadi ya warsha ipunguzwe maana inaleta mkanganyiko kwa washiriki na zinapungua ufanisi
·        Muda wa majadiliano ya plenary na kwenye warsha uongezwe
·        Huduma ya chakula  iboreshwe; na washiriki wapakuliwe chakula cha kutosha na maji ya kunywa yatolewe wakati wa chakula
·        Wana GDSS wajulishwe mapema kutokuwepo kwa uwezeshwaji wa nauli ili wajiandae
·        Taarifa za Tamasha zitolewe na kusambazwa miezi mitatu au zaidi kabla
·        Gharama za mauzo ya vikoi, tshirt, begi n.k. zijulikane mapema ili washiriki wajipange mapema kununua.



Ushiriki wa wana GDSS kwenye Tamasha lijalo uboreshwe vipi?:

·        Ratiba itoe nafasi zaidi kwa vikundi vya GDSS  kushiriki kuto mada  na kuonesha sanaa zao
·        Fursa za kujitolea (volunteers) zichukue wana GDSS w wengi zaidi
·        Kazi za maandalizi ya Tamasha kama vile usafi, kupaka rangi, useremala, mama lishe n.k. zitangazwe mapema ili wana GDSS wajipange na kuomba kuzifanya.
Makubaliano kuelekea Tamasha la Jinsia 2015:
·        Kuwe na  maandalizi ya mapema kwa wana GDSS  hususan semina maalum kwa wana GDSS kabla ya Tamasha ili waelewe vizuri mada kuu ya Tamasha, warsha zitakazokuwepo n.k ili ushiriki wao uwe na ufanisi zaidi

·        Tamasha la mwaka 2015, litakuwa mwaka wa Uchaguzi Mkuu Tanzania na huenda tukawa na Katiba mpya tayari, tutumie fursa hizi kuhakikisha linafana zaidi.

MWISHO


No comments: