Wednesday, January 9, 2013

TGNP Watoa Maoni Ya Mabadiliko Ya Katiba Mpya

Mwanachama wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Bi. Asseny Muro akitoa maoni ya mtandao huo kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo (Jumatano, Jan. 9, 2013), katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mwenyekiti wa TGNP Bi. Mary Rusimbi na Mjumbe wa Bodi ya mtandao huo Prof. Ruth Meena.

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jaji Joseph Warioba akiongea katika mkutano na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) uliolenga kupata maoni ya mtandao huo kuhusu Katiba Mpya leo (Jumatano, Jan. 9, 2013), katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam. Kulia kwa Jaji Warioba ni Bi. Ussu Mallya, Mkurugenzi Mtendaji wa mtandao huo, Prof. Ruth Meena 9Mjumbe wa Bodi ya TGNP) na Mwenyekiti wa TGNP Bi. Mary Rusimbi.

Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Dkt. Sengondo Mvungi akiongea katika mkutano na Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) uliolenga kupata maoni ya mtandao huo kuhusu Katiba Mpya leo (Jumatano, Jan. 9, 2013), katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni Wajumbe wengine wa Tume Bi. Mary Kashonda na Bi. Salma Moulidi.

TGNP pamoja na Tume Ya Mabadiliko ya Katiba katika Picha ya Pamoja
Mwananchama wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Bi. Subira Kibiga akitoa maoni ya mtandao huo kuhusu Katiba Mpya katika mkutano na Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo (Jumatano, Jan. 9, 2013), katika ofisi za Tume jijini Dar es Salaam. Wengine ni wananchama wenzake Bi. Diana Mwiru (kushoto) na Bi. Asseny Muro.


Na Deogratius Temba
MTANDAO wa Jinsia Tanzania (TGNP), leo wamekutana na Tume ya Kuratibu mchakato wa Katiba Mpya katika ofisi za Tume hiyo zilizoko jijini Dar es salaam.

TGNP waliongozwa na Mkurugenzi Mtendaji Usu Mallya, Mwenyekiti wa Bodi Mary Rusimbi naMkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Jinsia,  wakuu wa idara, wanachama, wafanyakazi na  wawakilishi wa vikundi vya kijamii vinavyoshiriki katika shughuli za harakati na TGNP.

Wakizungumza wakati wa kuwasilisha maoni yao kwa mtazamo wa Kijinsia, wanaharakati hao wamesema kuwa katiba mpya ni lazima itambue mchango wa wanawake katika maendeleo na uchumi wa taifa haswa kutambua shughuli za wanawake sizizo na kipato au sizizo rasmi. Haki za wanawake na usawa wa kijinsia katika mgawanyo wa rasilimali na nafasi za kutoa maamuzi serikali, haki za msingi za kijamii kama maji, afya, elimu, kilimo na ufugaji.

TGNP wameshauri Tume kuhakikisha inachukua masuala ya msingi yanayohusu wanajamii walioko pembezoni hasa wanawake na kuyaingiza kwenye katiba mpya ili changamoto ambazo zimekuwa zikimkabali Mwanamke ziondoke kabisa au kupungua baada ya kupatikana kwa katiba mpya. 

Kwa upande wake Mjumbe wa Tume Mary Kashonda, alisema kuwa  wanaharakati kutoka TGNP wana nafasi kubwa katika kuhakikisha wanatoa maoni yanayobeba sauti za wanawake walioko pembezoni hata wasio jua kusoma kutokana na ukaribu wao na jamii hasa wanawake wa pembezoni.

“Wanawake wengi huko vijijini hawawezi kuzungumza mbele ya wanaume, na ukiwaambia waandike hawawezi kwasababu hawajui kusoma na kuandika. Hili ni tatizo, Nyie TGNP mna fursa ya kukutana nao na kuwasilikiza   wakizungumza maoni yao ni muhimu sana…. Bila shaka mnayo”alisema Kashonda.

No comments: