Wednesday, February 10, 2010

Wawekezaji kunyang'anywa viwanda

WAWEKEZAJI wanaokiuka mikataba ya ununuzi wa viwanda watanyang’anywa, Serikali imelieleza Bunge.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Mary Nagu, amewaeleza wabunge kuwa, wawekezaji hao watanyang’anywa viwanda hivyo, watapewa wanaoweza kuwekeza kwa manufaa ya taifa.

Waziri Nagu ametoa msimamo huo wakati anajibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya, aliyedai kuwa, wawekezaji wengi wanakiuka mikataba ya ununuzi wa viwanda.

Kwa mujibu wa Nagu, Baraza la Mawaziri litaamua hatua za kuchukua endapo mwekezaji hatatekeleza mkataba wa mauzo.

No comments: