Wednesday, December 5, 2012

Udasa: Maslahi ya taifa kwanza

JUMUIYA ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Udasa), kimewataka wananchi kuweka siasa kando pale unapofika wakati wa kujadili masuala yanayohusu mustakabali wa taifa.Pia, Udasa imesema iwapo raslimali za taifa zitasimamiwa na kutumika vizuri kwa mapato yanayopatikana, wananchi wake wataondokana na ugumu wa maisha.

Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Udasa, Dk Francis Michael alipokuwa akizungumzia Kongamano la kujadili Mstakabali wa Taifa kwa miaka 50 ijayo ya uhuru, litakalofanyika chuoni hapo Desemba 9, mwaka huu.

Dk Michael alisema kongamano hilo halilengi kukuza mitazamo ya kisiasa, bali litakuwa na nia ya kulijenga taifa kwa vizazi vijavyo.

Alisema mada kuu ‘Uhuru Wetu na Mustakabali wa Taifa kwa Miaka 50 ijayo’, Makamu Mkuu wa chuo hicho, Profesa Rwekaza Mukandala kufungwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.

No comments: