Wanaharakati wakifuatilia mada kwa makini
Mwenyekiti wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Mary Rusimbi akiongea na waandishi wa habari wa kutoka vyombo mbalimbali kuhusu kuelekea kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani na miaka 50 baada ya uhuru na pia kutafakari juu ya maisha ya wanawake kwa kuzingatia elimu bora na kipato endelevu. Mary Rusimbi amebainisha kuwa siku ya wanawake duniani ni kutafakari miaka 100 ya maadhimisho ya siku ya wanawake duniani katika ustawi wa mwanamke wa kitanzania kiuchumi na kijamii, kuainisha michango, mapambano ya wanawake miaka 50 baada ya uhuru na kubainisha changamoto zinazowakabili kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni na kupanga mikakati ya baadae, kutandaa na kupashana habari.
No comments:
Post a Comment